Na GEOFFREY ANENE
WANAMICHEZO watakaowakilisha Kenya kwenye Olimpiki nchini Japan mnamo Julai 23 hadi Agosti 8 wamepokea chanjo yao ya pili ya Covid-19.
Wachezaji hao kutoka fani za taekwondo, raga ya wachezaji saba kila upande, ndondi na voliboli ya wanawake, walipokea chanjo hiyo Jumanne katika uga wa kimataifa wa Kasarani mjini Nairobi.
Waziri wa Michezo Amina Mohamed alikuwepo wakati wa zoezi hilo ambapo pia alipata kuzungumza na wachezaji na makocha wao kuhusu maandalizi yao ya michezo hiyo ya haiba itakayofanyika mjini Tokyo.”Tumepeana chanjo ya pili ilu kulinda wanamichezo wetu dhidi ya ugonjwa wa Covid-19,” Wizara ya Michezo ilisema Jumatano.
Kenya ilifaa kutoa chanjo ya pili mwezi Mei, lakini serikali ikaongeza kipindi cha kupeana dozi hiyo hadi wiki 12 baada ya India kupiga marufuku kusafirishwa kwa chanjo hiyo kufuatia ongezeko kubwa la virusi vya corona nchini.Chanjo ya kwanza ilitolewa kati ya Aprili 7 na Aprili 14.
Wakenya 90 wamefuzu kushiriki michezo ya Olimpiki wakiwemo pia waogeleaji Danilo Rosafio na Emily Muteti wanaofanyia mazoezi yao nchini Uingereza na Amerika wanakosoma katika Chuo Kikuu.
Timu ya marathon ilichaguliwa Februari ikiwa na washikilizi wa rekodi za dunia Eliud Kipchoge na Brigid Kosgei, miongoni mwa wengine. Ile ya riadha za uwanjani itajulikana Juni 17-19.

Author Profile
- I am a young Kenyan interested in new media and dissemination of news and information as it unfolds.
Latest entries
Uncategorized2023.03.20CS Murkomen Summoned to Court Over failure to Construct public toilets on highways
News2023.03.20Kisumu Protesters Overpower Police Force
News2023.03.20Gachagua Pleads With Raila to Call off Protest
News2023.03.19Andrew Kibe calls on Azimio Coalition politicians to bring their kids on Monday