[ad_1]
– Vifo vya watu vimeongezeka hadi 2,724 baada ya wagonjwa wengine 17 kuangamizwa na maradhi hayo hatari katika tarehe tofauti
– Kagwe alisema kuwa kuna wagonjwa 1,311 waliolazwa kwa sasa katika hospitali mbali mbali kote nchini
– Jumla ya wagonjwa 188 wako ICU, wagonjwa 137 wanaongezewa oksijeni
Mnamo Ijumaa, Aprili 30 Kenya ilirekodi visa vingiine 497 vya Covid-19, na kufikisha jumla ya idadi ya wagonjwa nchini kutimia 159,318, Waziri wa Afya Mutahi Kagwe alisema.
Waziri katika taarifa yake kwa vyombo vya habari alidokeza kuwa visa hivyo vilithibitishwa baada ya sampuli 5,117 kupimwa ambapo sasa asilimia ya maambukizi ni 9.7.
Habari Nyingine: Mchekeshaji Jemutai Asema Amelemewa na Maisha, Aomba Wakenya Wamsaidie
Source: UGC
Tangu mwezi Machi 2020 idadi ya sampuli zilizopimwa imefika 1,669,552.
Vifo vya watu vimeongezeka hadi 2,724 baada ya wagonjwa wengine 17 kuangamizwa na maradhi hayo hatari katika tarehe tofauti.
Kagwe alisema kuwa kuna wagonjwa 1,311 waliolazwa kwa sasa katika hospitali mbali mbali kote nchini. Wagonjwa wengine 6,650 nao wanahudumiwa wakiwa nyumbani.
Habari Nyingine: Mweka Hazina wa KNUT John Matiang’i Astaafu Mapema Kushughulia Familia Yake
Jumla ya wagonjwa 188 wako ICU, wagonjwa 137 wanaongezewa oksijeni.
Wakati uo huo, wagonjwa 441 wameripotiwa kupona ugonjwa ambapo 366 kati ya walikuwa wakihudumiwa nyumbani nao 75 walikuwa wakipata matibabu katika hospitali mbali mbali nchini.
Habari Nyingine: Kitui: Utani wa Jamaa Katika Karamu Wamsababishia Mashaka
Aidha jumla ya idadi ya wagonjwa walipata nafuu nchini Kenya imegonga 108,565.
Kwa upande wa chanjo, Kagwe alisema watu 876,708 walikuwa wamechajwa kufikia Ijumaa, 271,079 kati ya wale walio na umri wa chini ya miaka 58, wahudumu wa afya 157,211, walimu 135,957 na maafisa usalama 73,544.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Soma taarifa zaidi kwa TUKO.co.ke.
Source: Tuko
[ad_2]
Source link