[ad_1]
Shughuli za kuwaokoa wafanyakazi zaidi ya kumi waliokwamba kwenye jengo mpya la makao makuu ya bunge la kaunti ya Nyamira zinaendelea.
Habari Nyingine: Raila Akosa Kuhudhuria Maombi ya Kitaifa Badala Yake Amtembelea Mukhisa Kitui Nyumbani Kwake
Source: UGC
Habari Nyingine: COVID-19: Wizara ya Afya Yatangaza Maafa 11, Maambukizi 341
Jengo hilo liliporomoka Alhamisi, Mei 27 na inahofiwa kwamba huenda zaidi ya watu kumi wamepoteza maisha yao kwenye mkasa huo.
Wafanyakazi watatu walikimbizwa katika hospitali ya rufaa ya Nyamira baada ya maafisa wa polisi na wahudumu wa afya kufika katika eneo la mkasa.
Wakazi waliwasaidia polisi pamoja na maafisa wa shirika la msalaba mwekundu kuwaokoa waathiriwa, hata hivyo, idadi kamili haswa ya waliokwama kwenye jengo hilo haijabainika.
Habari Nyingine: Bintiye DP Ruto, June Afunga Ndoa na Mahabubu wake Alex Ezenagu
Ripoti za kuaminika ziliarifu kwamba, huenda mvua kubwa ambayo inaendelea kunyesha eneo hilo ndio ilisababubsha kuporomoka kwa jengo hilo linalokisiwa kugharimu mamilioni ya pesa.
Aidha, Imeripotiwa kwamba maafisa wa polisi wamekuwa na wakati mgumu kuwatawanya wakazi wenye hamaki waliotaka kumuadhibu mkandarasi wa jengo hilo.
Shahidi mmoja alisema kwamba alighabisha baada ya kuona wajenzi wakiendelea kujenga licha ya jengo hilo kuporomoka, hawakujali usalama wao.
Jengo hilo lilikuwa limefikia orofa ya pili na lilikuwa linaelekea kukamilikia kwenye orofa ya tatu.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke
Source: Kenya Breaking News Today
[ad_2]
Source link