[ad_1]
– Mbunge wa Sabari Alfred Agoi alielezea imani yae kwamba Musalia Mudavadi ndiye kiongozi imara wa kuliendesha taifa
– Kiongozi wa ANC alitaja uchumi kama maeneo ya kipaumbele ambayo atazingatia ikiwa atashinda urais mnamo 2022
– Mnamo Julai 2020, Kamati Kuu ya ANC ilifanya kikao na kuafikiana kwa pamoja kwa Mudavadi ndiye atakayepeperusha bendera ya chama hicho 2022
Kiongozi wa chama cha Amani National Congress (ANC) Musalia Mudavadi ametaja uchumi kama maeneo ya kipaumbele ambayo atazingatia katika kipindi chake cha kwanza cha urais.
Habari Nyingine: Tunapoweka Mikakati ya Kuboresha Kilimo Tusisahau Kuinua Maendeleo ya Vijijini

Source: Twitter
Makamu huyo wa zamani wa rais na ambaye pia alikuwa Waziri wa Fedha ana hakika kwamba kutokana na uzoefu na ujuzi aliopata wakati akishikilia nyadhifa hizo ni tosha kukabiliana na suala la uchumi wa taifa.
Wanajeshi wake wa kisiasa wakiongozwa na mbunge wa Sabatia Alfred Agoi na Sakwa Bunyasi wa Nambale pia walielezea imani yao kwamba mwanasiasa huyo mzoefu ndiye kiungo aliyekosekana katika uongozi wa Kenya.
“Ni wazi kwamba macho yote sasa yanamtazama Musalia Mudavadi. Taifa linahitaji kiongozi ambaye atarekebisha uchumi wa taifa na kuuimarisha tena. Hiyo ni mojawapo ya wesa zake kuu atakapoingia uongozini,” Agoi alisema.
Habari Nyingine: Ben Githae: Uhuru na Ruto Walinipa Minofu Minono Kwa Ajili ya Tano Tena
Kwa upande wake, Bunyasi alisema kaunti, tofauti na maeneo bunge, zimepewa sababu zote nne za uzalishaji ambazo zinaweza kutumika kwa ukuaji uchumi, ambayo ni nguzo muhimu katika manifesto ya ANC.
“Kama chama cha ANC, tunazingatia kujenga uongozi ambao utatoa ubora kama huo kwa ukuaji kamili katika kaunti zetu,” alisema.
Mnamo Julai 2020, Kamati Kuu ya ANC ilifanya kikao na kuafikiana kwa pamoja kwa Mudavadi ndiye atakayepeperusha bendera ya chama hicho 2022.
Habari Nyingine: Limuru: Wezi wa Usiku Wachomoka na Kengele Kubwa ya Kanisa Iliyonunuliwa Ulaya
Katibu mkuu wa zamani wa ANC Barrack Muluka alithibitisha chama hicho kitaendesha tu kura za mchujo za chama kwa viti vingine isipokuwa ile ya mgombea urais.
Kufuatia hilo, Muluka alisema Mudavadi sasa yuko huru kutafuta uungwaji mkono kutoka kwa wenzake wenye nia moja na ambao wangependa kuunda muungano wa siasa.
Kiongozi huyo wa ANC alidokeza awali alikuwa tayari kufanya kazi na mwanasiasa yeyote akiwemo Naibu Rais William Ruto maadamu angeunga mkono zabuni yake ya urais.
Read ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Source: Tuko.co.ke
[ad_2]
Source link