[ad_1]
– Jemtai ana watoto wawili ambao ni wenye sura za kuvutia
– Wawili hao wanafanana naye kama shilingi kwa ya pili na hufurahia kuwaanika mtandaoni
– Jemtai alifichua kuwa Prof Hammo ni mpenziwe lakini ameingia mafichoni na hatoi usaidizi
Mchekeshaji Jemutai Ijumaa alisambaa kwenye mitandao baada ya kufungua roho kuwa maisha yemekuwa magumu sana.
Source: Instagram
Mchekeshaji huyo alipata umaarufu wakati wa kipindi cha Churchill Show ambapo aliwaacha wengi wakivunja mbavu.
Hata hivyo, tangu janga la Covid-19 libishe, wasanii wengi wameteseka na Jemtai alifichua yeye ni mmoja wao.
Msanii huyo ni mama wa watoto wawili na kwa kweli Mungu amembariki na damu safi kwani picha hizi ni za kutamaniwa sana.
Amebarikiwa na msichana na mvulana na aliwahi kusema sasa amemaliza kibarua cha ‘kujaza dunia’
“Nimekafunga. Niko na watoto wawili kama mamangu tu. Alikuwa na mimi na ndugu yangu,” alisema msanii huyo.
Ukipita kwenye ukurasa wa Instagrama wa msanii huyo, ni wazi kuwa yeye ni mama wa kupendeza.
Ana watoto ambao wanavutia na kufanya wengi kutamani kuwa wazazi angalau wafurahia kuitwa baba au mama.
Watoto hao pia wanafanana na mama yao kiwango cha shilingi kwa ya pili.
Amekuwa akipakia safari yake ya ulezi mtandaoni kwa wale ambao huenda wakataka kujifunza jambo.
“Kuanzia Chebaibai ajue kuita Mum,Weeeh.. kuanzia asubuhi ni mum,mum ,muuuuuuum. Hadi najificha ndo nipumzike kuitika. Mimi aki huyu atanimalizia jina,” alaindika wakati mmoja.
Aliwahi kukiri kuwa safari ya ulezi si rahisi kwa kina mama kwani mengi, ikiwamo mwili kubadilika, humfanyia mwanamke.
“Naendelea kumtamani huyu mama ambaye alitekwa na ulezi na kiu cha kuendeleza ndoto zake kiwangi cha kujisahau. Sasa yuko kwenye safari ya kujipenda na kukua ili kuweza kufanya yote. Nasherekea kina mama wote wanaofanya hivyo, sisi ni kiboko chao, si rahisi lakini tunajaribu,” alisema.
Jemtai Ijumaa Aprili 30 aliwaomba wanamtandao usaidizi baada ya kufichua kuwa huenda akafungiowa nyumba baada ya kushindwa kulipa.
Baba wa mwanawe, ambaye alitambulika kama Profesa Hamo, alisema aliingia mafichoni na hatoi usaidizi wa ulezi.
READ ENGLISH VERSION
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke
Source: Tuko.co.ke
[ad_2]
Source link