[ad_1]
– Mchekeshaji Jemutai amesema amekuwa mpweke au tusema ‘Single Mum’ kwa muda wa mwaka mmoja
– Kulingana na mchekeshaji huyo, maisha yamekuwa magumu tangu mlipuko wa virusi vya COVID-19 uliporipotiwa nchini Machi 2020
– Jemutai ana watoto wawili ambao anawalea pekee, kulipa bili na pia kodi ya nyumba, mumewe alimtema baada ya maisha kuwa ghali
Mchekeshaji wa kipindi cha Churchill Show Stella Jemutai Koitie almaarufu Jemutai amewataka mashabaki wajitolee kumsaidia pamoja na watoto wake kukimu maisha.
Jemutai amepitia maisha magumu tangu mume wake alipomuacha mwaka jana maisha yalipoanza kuwa mangumu.
Akizungumza na TUKO.co.ke, Jemutai alisema”, Nimekuwa Single Mum kutoka mwaka wa 2020, nilikuwa naishi na baba ya watoto wangu kutoka mwaka wa 2018 lakini aliondoka mwaka jana.
” Nina watoto wawili, mmoja ana umri wa miaka mitano na mwingine anatimia mwaka mmoja na miezi sita,” Jemutai alisema Ijuma Aprili 30.
Jemutai amekuwa akitangazie kampuni kadhaa kama balozi na kwa sasa amesema maisha yamekuwa ghali mno , hapati kandarasi tangu mlipuko wa virusi vya COVID-19 uliporipotiwa nchini.
Kulingana na mchekeshaji huyo, kuomba usaidizi imekuwa suala ambalo limekuwa likimtatiza lakini kwa sasa ameamua kufanya hivyo kwa ajili ya maisha ya watoto wake.
” Nikipata kampuni yoyote itakayonipa nafasi ya kufanya kazi ya ubalozi, nitasaidika sana kwa sababu nina mashabiki wengi mitandaoni, hizo dhinisho zitanisaidia kuwalea watoto wangu,” Jemutai aliongezea.
Source: Tuko.co.ke
[ad_2]
Source link