[ad_1]
– Katumba alipigwa risasi na watu wasiojulikana Jumanne, Juni 1 akiwa katika barabara ya Kisota eneo la Kisaasi
– Binti ya jenerali huyo wa polisi aliuawa kwenye shambulizi hilo baada ya kupigwa risasi
– Rais Museveni ameahidi kwamba waliohusika kwenye mauaji hayo watachukuliwa hatua kali za kisheria
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amekashifu vikali jaribio la mauaji kwa aliyekuwa waziri wa kazi na uchukuzi Jenerali Katumba.
Katumba Wamala ambaye ni jenerali katika kikosi cha ulinzi alipigwa risasi na watu wasiojulikana Jumanne, Juni Mosi katika barabara ya Kisota eneo la Kisaasi.
Bintiye Wamala ambaye alikuwa akisafiri kwenye gari moja na babake alipigwa risasi na kufariki dunia papo hapo.
Rais Yoweri Museveni aliwataja washambuliaji hao kama watu wasio na utu na ameahidi kwamba serikali yake itakabiliana nao vilivyo kisheria.
Museveni aliwalinganisha washambulianaji hao na nguruwe.
” Nguruwe hao ambao hawathathmini maisha, walimpiga risasi Jenerali Katumba na Bintiye pamoja na dereva wake ambao walifariki dunia, tunaomboleza vifo vyao… Kwa sasa tuna habari kuhusu waliohusika na mauaji hayo”. Museveni alisema.
Museveni alimkashifu mlinzi wa Katumba kwa kufyatua risasi hewani, ila badala yake angewafyatulia washambuliaji hao na kuwauwa papo hapo.
” Mlinzi huyo hangefyatua risasi hewani. Angewauwa washambuliaji hao, kwa sasa tungelikuwa na gaidi ambaye ni maiti kuliko yule anaye tutishia,” Museveni aliongezea.
Akizungumza akiwa hospitalini, Katumba alimshukuru Mungu kwa kuyaokoa maisha yake lakini pia aliwaomba wananchi watulie na wazidi kuombea familia yake inapopitia wakati huu mgumu wa majonzi.
” Temmpoteza Brenda lakini ni kwa ajili ya mpango wa Mungu,hakufanya chochote kibaya lakini washambuliaji wake wamefanya hivyo, msiwe na shaka, sina majeraha mabaya nitakuwa sawa,”Katumba alisema.
Source: Tuko
[ad_2]
Source link