Home » Vihiga: Aburuta Maiti ya Mamake Barabarani Baada ya Mochari Kukataa Kuhifadhi ▷ Kenya News
News

Vihiga: Aburuta Maiti ya Mamake Barabarani Baada ya Mochari Kukataa Kuhifadhi ▷ Kenya News

Vihiga: Aburuta Maiti ya Mamake Barabarani Baada ya Mochari Kukataa Kuhifadhi ▷ Kenya News

[ad_1]

Hifadhi ya Maiti ya Hospitali ya Rufaa ya Vihiga imemulikwa baada ya mwanamke mmoja kulalamika kuwa ilikataa kuhifadhi maiti ya mama yake.

Vihiga: Mrembo Aburuta Maiti ya Mamake Barabarani Baada ya Hospitali Kukataa Kuhifadhi
Hospitali ya Rufaa ya Vihiga imemulikwa kwa kukataa maiti.Picha:UGC.
Source: UGC

Mwanamke huyo asiyejulikana alisema mama yake alilazwa hospitalini humo Jumatatu, Mei 31, lakini alikata roho Jumanne, Juni 1 mwendo wa saa tano asubuhi.

Akilalamika katika video ambayo imesambaa kwenye mtandao wa Facebook, alisema wahudumu wa mochari walikataa kuhifadhi mwili huo.

Habari Nyingine: Mfungwa Atolewa Misumari 30 Tumboni, Kalamu Nne na Sindano

Sababu za mwili huo kukataliwa bado ni kitendawili na hivyo kumlazimu mwanamke huyo kuvuta mwili wa mama yake barabarani akitaka marehemu atendewe haki.

Kisa hicho kinakujia miezi michache baada ya kioja kushuhudiwa katika barabara kuu ya Vihiga wakati mwili ambao ulikuwa unasafirishwa nyumbani kuzikwa “kukataa”.

Duru ziliarifu kuwa mama huyo aliaga dunia baada ya kuugua kwa muda mfupi na alikuwa anapelekwa nyumbani kwake kuzikwa wakati mambo yalikwenda segemnege.

Habari Nyingine: Tharaka Nithi: Buda Azua Kisanga Baada ya ‘kudinda’ Kuzikwa

Katika video iliyochapishwa na NTV, gari lililokuwa limebeba mwili huo lilisimama ghafla kati kati ya barabara hiyo yenye shughuli nyingi na kusababisha msongamano mkubwa wa magari.

Wakazi na madereva walioshuhudia tukio hilo walikuwa na simulizi za kushtua jinsi mwili huo utasafirishwa baada ya kisa hicho cha kushangaza.

Wengi walisema si mara ya kwanza tukio kama hilo kutokea katika eneo hilo huku miili nyingi ikikataa kuzikwa maeneo fulani kwa sabababu kadha.

Katika kisa hiki, mwanamke huyo anaripotiwa kuhusika kwenye mgogoro wa kinyumbani na mume wake kila mara na kifo chake kilitokea akiwa ameondoka kwenye ndoa hiyo.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Source: Tuko.co.ke

[ad_2]

Source link