[ad_1]
– Miili mitatu tayari imepatikana katika maeneo ya Marang’a, Thika na Mathioya
– Maswali yameibuka ni vipi waliotekeleza mauaji waliweza kusafiri hadi maeneo hayo kutupa miili hiyo ilhali kuna kafyu ya kutoingia kaunti zingine
– Familia inataka jamaa anayejulikana kama Erico kusakwa kwani ndiye alitumia mtandao kuripoti lilipokuwa gari lao aina ya Mark X
Maswali yameibuka kuhusu mauaji ya jamaa wanne wa Kitengela ambao walitoweka Aprili 19 na kisha miili yao kupatikana sehemu mbali mbali.

Source: UGC
Tayari miili mitatu imepatikana maeneo ya Murang’a, Thika na Mathioya ikiwa imetupwa kwenye mito.
Mwili wa tatu ambao umetambulika kama wa Elijah Ochieng ulipatikana ukiwa kwenye gunia huku ikiibuka mauaji yake yalikuwa ya kinyama.
Ripoti zinaarifu kuwa baadhi ya sehemu za mwili zilikosekana kuonyesha huenda aliteswa vibaya kabla ya kuuawa.
Habari Nyingine: Magazeti Ijumaa: Huenda Shule Zisifunguliwe, Wanafunzi Kuendelea Kukaa Makwao
Kulingana na familia, miili iliyotambuliwa kufikia sasa ni ile ya Benjamin Imbai, Jack Ochieng na Elijah Obuong.
Polisi wanaendelea na uchunguzi kuhusu alipo Brian Oduor ambaye alikuwa na watatu hao ingawa matumini ya kupatikana akiwa hai.
Nduguye Jack, Michael Amollo, alisema polisi wanafaa kumsaka jamaa aliyewajulisha kuhusu kutoweka kwa wanne hao kupitia mtandao.
Habari Nyingine: Wakili Cliff Ombeta Sasa ni ‘Hasla’ Aanza Rasmi Kutangatanga

Source: UGC
Jamaa huyo ametambulika kama Erico na inadaiwa alifahamisha familia lilipokuwa gari ambalo wanne hao walikuwa wakitumia Jumapili Aprili 19 kabla ya kutoweka.
“Hatuelewi ni kwa nini polisi hawajafuatilia mazungumzo yao na pia kumsaka jamaa huyu anajiita Erico,” Amollo alisema.
Kama TUKO.co.ke ilivyoripoti awali, wanne hao waliripotiwa kutoweka baada ya kushiriki chakula cha mchana katika klabu moja Kitengela.
Habari Nyingine: DP Ruto Asisimka Baada ya Rais wa Marekani Kuhubiri Injili ya Wheelbarrow
Ripoti za kuwa walishiriki uhalifu ziliibuka pia huku kutoweka kwao kukihusishwa na polisi au tofauti ndani ya genge fulani.
DCI walisema Benjamin Imbai alikuwa amehusishwa na wizi wa KSh 900, 000 mwaka uliopita baada ya kunaswa na wengine wakivunja gari na kuhepa na noti hizo.
Hata hivyo, familia imeshikilia wanne hao walikuwa ni watu wangwana kwenye jamii waliojitafutia riziki kwenye biashara ya uuzaji wa magari.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Tazama habari za TUKO hapa
Source: Tuko.co.ke
[ad_2]
Source link