[ad_1]
– June Ruto anatarajiwa kufunga pingu za maisha na mpenzi wake raia wa Nigeria Alhamisi, Mei 27 nyumbani kwa babake mtaani Karen
– Sherehe hiyo itahudhuriwa na wageni waalikwa pekee, wengi wakiwa waandani wa karibu wa naibu Rais William Ruto
– Wakwe wa DP Ruto walimtembelea nyumbani kwake kwa mazungumzo ya mahari kwa ajili ya binti yake June Jumamosi, Mei 8
Bintiye kifungua mimba wa naibu Rais William Ruto June Ruto anatarajiwa kufanya harusi na mpenzi wake raia wa Nigeria Alexander Ezenagu Alhamisi, Mei 27.
Habari Nyingine: Kiambaa: DP Ruto Akutana na Aliyekuwa Mgombea wa PEP Kumaliza Uhasama

Source: Twitter
Habari Nyingine: Shangwe Baada ya Mzee Aliyetoweka Nyumbani Kurejea Miaka 57 Baadaye
Sherehe ya harusi inajiri takribani majuma matatu baada ya wakwe wa DP Ruto kumtembelea nyumbani kwake kwa mazungumzo ya mahari.
Taarifa za kuaminika zimearifu kwamba harusi hiyo itafanyika nyumbani kwa Ruto mtaani Karen na wageni waalikwa pekee ndio watakaoruhusiwa kuhudhuria sherehe hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa za The Standard, wandani wa karibu wa Ruto ndio watakuwa miongoni mwa wageni mashuhuri.
Ezanugu ni wakili msaidizi katika chuo kikuu cha Hamad Bin Khalifa mjini Doha, Dubai.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke
Source: Breaking News
[ad_2]
Source link