Home » COVID-19: Wagonjwa 198 Walazwa ICU Huku Asilimia ya Maambukizi Kenya Ikishuka ▷ Kenya News
News

COVID-19: Wagonjwa 198 Walazwa ICU Huku Asilimia ya Maambukizi Kenya Ikishuka ▷ Kenya News

COVID-19: Wagonjwa 198 Walazwa ICU Huku Asilimia ya Maambukizi Kenya Ikishuka ▷ Kenya News

[ad_1]

– Jumla ya waliopoteza maisha yao kutokana na makali ya COVID-19 imeongezeka hadi 2,688 baada ya wagonjwa wengine 23 kufariki dunia

– Waziri Kagwe alisema wagonjwa 1,300 wamelazwa katika hospitali mbali mbali nchini

Kenya imerekodi visa vingine 834 vya Covid-19, kutokana na sampuli ya 8,498 zilizopimwa katika saa 24 zilizopita ambapo asilimia ya maabukizi imepungua hadi 9.8.

Katika visa hivyo, wagonjwa 805 ni Wakenya nao 29 ni raia wa nchi za kigeni. 499 ni wanaume na 335 ni wanawake. Mgonjwa mwenye umri mdogo zaidi ni mtoto wa siku kumi na nne naye mkongwe zaidi zaidi ana miaka 100.

Habari Nyingine: Waziri Kagwe apiga marufuku safari za ndege kutoka Kenya kuelekea India

COVID-19: Wagonjwa 198Walazwa ICU Huku Asilimia ya Maambuzki Ikishuka
Waziri wa Afya Mutahi Kagwe akihutubu hapo awali. Picha: MoH.
Source: UGC

Kwenye taarifa yake ya mano Jumatano, Aprili 28, Waziri wa Afya Mutahi Kagwe alisema kuwa wagonjwa 579 walipata nafuu kutokana na ugonjwa huo, 293 wlikuwa wakihudumiwa nyumbani nao 286 kutoka vituo vya afya mbali mbali.

Jumla ya wagonjwa waliopona nchini imefika 107,882 ambapo 78,500 kati yao walikuwa wakihudumiwa nyumbani nao 29,382 walikuwa katika vituo mbali mbali vya afya.

Wakati uo huo vifo 23 viliripotiwa kwa zaidi ya saa ishirini na nne zilizopita. Visa viwili vilitokea katika saa 24 zilizopita, 15 kati ya waliofariki dunia walipoteza maisha yao katika tarehe tofauti ndani ya mwezi mmoja uliopita.

Habari Nyingine: Wapelelezi Wanasa Sarafu Bandia za KSh 802.4 Milioni Mtaani Kilimani

Vifo sita navyo vilitekodiwa wakayi wa ukaguzi wa vituo vya afya. Kwa sasa idadi ya waliofariki dunia kutokana na makali ya virusi vya corona imeongezeka hadi 2,688.

Jumla ya wagonjwa 1,300 kwa sasa wamelazwa katika vituo mbali mbali vya afya nchini kote, wakati wagonjwa 6,978 nao wametengwa manyumbani mwao.

Wagonjwa 198 wako katika chumba cha wagonjwa mahututi (ICU), 134 kati yao wanaongezewa oksijeni ya ziada. Wagonjwa 29 wanachunguzwa kwa karibu na madaktari.

Habari Nyingine: Raila, Ruto Wamuomboleza Mwanahabari Mkongwe Philip Ochieng’

Kufikia leo, jumla ya watu 853,081 wamepewa chanjo dhidi ya ugonjwa wa Covid-19 nchi nzima.

Kati yao 494,278 wana umri wa miaka 58 na zaidi, Wafanyakazi wa Afya 155,294, walimu 131,905 nao Maafisa Usalama 71,604.

Kuanzia Aprili 26, 2021, jumla ya dozi 1,099,000 zilikuwa zimesambazwa kwa bohari za mkoa kote nchini na kuacha usawa wa dozi 21,000 katika maduka ya Chanjo kuu ya Kitengela.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Source: Tuko

[ad_2]

Source link