Home » COVID-19: Wakenya Waanza Safari za Mashinani Baada ya Rais Kufungua Kaunti 5 ▷ Kenya News
News

COVID-19: Wakenya Waanza Safari za Mashinani Baada ya Rais Kufungua Kaunti 5 ▷ Kenya News

COVID-19: Wakenya Waanza Safari za Mashinani Baada ya Rais Kufungua Kaunti 5 ▷ Kenya News

[ad_1]

Saa chache baada ya Rais Uhuru Kenyatta kufungua kaunti tano zilizofungwa Machi 26 kwa ajili ya kudhibiti maambukizi ya virusi vya COVID-19, mamia ya Wakenya wameshaanza safari za kwenda mashinani.

Rais Uhuru Kenyatta alikuwa amefunga kaunti za Nairobi, Machakos, Kiambu, Nakuru na Kajiado.

Hata hivyo, TUKO.co.ke imeweza kubaini kwamba barabara za Nairobi kuelekea Naivasha na Mahi Mahiu zimeshuhudia msongamano mkubwa wa magari.

Wakenya wengi walikiri kwamba walikuwa wamekwama katika kaunti tofauti baada ya Rais kutangaza kufungwa kwa kaunti hizi.

Rais pia ameruhusu mikahawa na baa katika kaunti hizo tano kufunguliwa ili kuendelea kuchapa kazi.

Wakazi wa kaunti hizi tano sasa wameruhusiwa kunywa pombe kuanzia mchana hadi saa moja jioni, sasa za kafyu ni kutoka saa kumi asubuhi hadi saa nne usiku.

Shughuli za ibada pia zitarejelewa ila agizo ni kuwa waumini wawe ni theluthi moja pekee kwa kila kikao.

Source: Tuko News

[ad_2]

Source link