Home » Jumatatu, Mei 31: Watu 15 Zaidi Waangamizwa na COVID- 19, Wengine 88 Wapatikana na Virusi ▷ Kenya News
News

Jumatatu, Mei 31: Watu 15 Zaidi Waangamizwa na COVID- 19, Wengine 88 Wapatikana na Virusi ▷ Kenya News

[ad_1]

– Kufikia sasa watu 116, 847 wamepona kutokana na ugonjwa wa corona tangu kisa cha kwanza cha maambukizi kiliporitiwa nchini mwezi Machi mwaka wa 2020

– Waziri Kagwe ametangaza kwamba watu wengine 88 wamepatikana na virusi vya covid-19 huku watu 15 zaidi wakipoteza maisha Jumatatu, Mei 31

– Kwa jumla idadi ya maambukizi kote nchini kwa yamefikia 170, 735

Wizara ya Afya imetangaza kwamba watu wengine 88 wamepatikana na virusi vya COVID-19 baada ya sampo 1,1668 kufanyiwa vipimo chini ya saa 24 zilizopita.

Habari Nyingine: West Pokot: Mwanamke Aliyefanya Harusi na Roho Mtakatifu Aelekea Uganda kwa Fungate

Jumatatu, Mei 31: Watu 15 Zaidi Waangamizwa na COVID- 19, Wengine 88 Wapatikana na Virusi
Waziri Kagwe ametangaza kwamba watu wengine 88 wamepatikana na virusi vya covid-19 huku watu 15 zaidi wakipoteza maisha Jumatatu, Mei 31.Picha: MoH
Source: Facebook

Habari Nyingine: Kamata Hao! Atwoli Asema Kuhusu Waliobomoa Bango la Barabara Yake Kileleshwa

Kwa jumla idadi ya maambukizi kote nchini kwa yamefikia 170, 735.

Kwenye hotuba yake kwa taifa Jumatatu, Mei 31, Waziri wa afya Mutahi Kagwe pia alitangaza kwamba watu wengine 15 wamepoteza maisha yao kutokana na makali ya maradhi hayo.

Kaunti ya Nairobi inaendelea kuongoza kwa idadi ya maambukizi ikiwa na visa 30, ikifuatwa na kaunti ya Nandi 10, Turkana 7, Kericho 6, Mombasa 5, Kirinyaga 4, Kakamega, Kiambu na Uasin Gishu, Garissa, Kajiado, Nakuru zikiwa na visa 3 kila moja na Siaya na Kisumu visa viwili kila moja.

Kisii, Laikipia, Machakos, Bungoma, Meru, Migori na Pokot Magharibi vikiwa na kisa kimoja kimoja.

Habari Nyingine: Siaya: Rais Uhuru Alipa Karo ya Watoto Maskini Waliomupa Maji Masafi ya Kunywa

Kagwe pia alitangaza kwamba idadi ya watu waliopona kutokana na virusi hivyo imefikia 116, 847 baada ya wengine 71 kupona, 64 walikuwa chini ya utunzi wa nyumbani ilhali 7 walikuwa wamelazwa katika hospitali mbali mbali.

Wagonjwa wengine 1,237 wamelazwa katika hospitali mbali mbali ilhali 4, 661 wamewekwa chini ya mpango wa utunzi wa nyumbani.

Kulingana na takwimu za wizara hiyo, wagonjwa 93 wamo katika vyumba vya ICU, kati ya 21 wakiwa kwenye ventileta, 55 oksijeni na 17 wakichunguzwa.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Subscribe to watch new videos

Source: Kenyan Breaking News

[ad_2]
Source link