[ad_1]
Hatimaye serikali ya Rais Uhuru Kenyatta imetangaza kuondolewa kwa marufuku ya safari za ndege kuingia na kutoka nchini Somalia.
Habari Nyingine: Magazeti Jumatano Juni 9: Mambo Matatu Ambayo Yanampa Uhuru ‘Stress’ Katika Ikulu

Source: UGC
Habari Nyingine: Rais wa Ghana Amuomba Nyota wa Chelsea Hudson-Odoi Abadilishe Uraia
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa wizara ya Mambo ya nje, uamuzi huo uliafikiwa kwa lengo la kuhalalisha rasmi uhusiano wa kibiashara kati ya nchini hizi mbili.
“Serikali ya Kenya imezingatia maombi yaliyofanywa na imeamua kufungua tena anga ya Kenya kwa ndege zote zinazotokea Somalia na kutoka Kenya kwenda Somalia,” ilisema taarifa hiyo.
Wizara hiyo imeshinikiza kwamba masharti ya kupambana na virusi vya COVID-19 kwa wasafiri kutoka nchi hizi mbili yatazingatiwa ipasavyo.
Wasafiri watahitajika kuwasilisha hati zinazoonyesha kwamba hawana maambukizi ya virusi vya covid-19.
Habari Nyingine: Willy Paul Afichua Sababu Iliyomfanya Aache Kufanya Miziki za Injili
Ni takribani mwezi mmoja tangu serikali ya Kenya ilipofunga anga zake, aidha kumekuwepo na mvutano kati ya nchi hizi mbili kwa muda.
” Watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano wataruhusiwa kuingia bila hati za kuonyesha iwapo wana maambukizi au la,” Sehemu Nyingine ya taarifa hiyo ilisoma.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke
Source: Tuko
[ad_2]
Source link