Home » Kilabu Walimoonekana Jamaa 4 Kabla ya Kutoweka Chakanusha Walikula Chamcha Eneo Hilo ▷ Kenya News
News

Kilabu Walimoonekana Jamaa 4 Kabla ya Kutoweka Chakanusha Walikula Chamcha Eneo Hilo ▷ Kenya News

Kilabu Walimoonekana Jamaa 4 Kabla ya Kutoweka Chakanusha Walikula Chamcha Eneo Hilo ▷ Kenya News

[ad_1]

– Usimamizi wa Klabu ya Enkare ulikanusha ripoti kwamba watu hao wanne waliopotea walikula cha mchana muda mfupi kabla ya kutoweka

– Wasimamizi wa baa hiyo walisema baada ya kukagua picha za CCTV kutoka Jumatatu, Aprili 19, wanne hao hawakuonekana wala gari lao la Toyota Mark X

– Wapelelezi walisema gari hilo lilipatikana likiwa limefunguliwa na kuongeza kuwa simu za wanaume hao zilikuwa zimezimwa karibu na Everest Park, Barabara ya Mombasa

Usimamizi wa kilabu huko Kitengela ambapo wanaume wanne waliosemekana walikula chakula cha mchana kabla ya kutoweka kwa kwa njia ya utata wamekanusha ripoti kwamba walikuwa huko.

Habari Nyingine: Kenya Inahitaji Musalia Mudavadi kama Rais Atakayeimarisha Uchumi, Mbunge Agoi Asema

Kilabu Ambacho Jamaa 4 Walionekana Mara ya Mwisho Chakana Walikula Chamcha
Wanaume hao walitoweka baada ya kula chamcha katika kilabu mtaani Kitengela mnamo Jumatatu, Aprili 19. Picha: The Standard.
Source: UGC

Elijah Obuong, 35, Brian Oduor, 36, Jack Ochieng, 37 na Benjamin Imbai, 30, walionekana mwisho mchana wa Aprili 19 wakati wakila chakula cha mchana pamoja katika Club Enkare.

Kulingana na ripoti ya TV47, meneja wa baa hiyo Bernand Monda alisema walikagua picha zao za CCTV Jumatatu, Aprili 19 lakini hawakuwaona wanaume hao.

“Baada ya kukagua picha zetu za CCTV, hatukuona yoyote yao au gari. Tangu kufungwa kwa baa, hatujawahi kuuza pombe kwa mtu yeyote. Hapa wateja wananunua chakula na kuondoka,” alisema.

Habari Nyingine: Picha Muruwa za Mwanamke Aliyedaiwa Kushiriki Ngono na Askofu Stanley Ntagali

Kulingana na meneja wa teknolojia kilabuni humo Joel Mukuru, ni mtu mmoja tu aliyeonekana akiegesha gari lake karibu na baa hiyo kabla ya kuondoka tena.

“Gari hilo lilikuwa tofauti na lile la Toyota Mark X,” alisema.

Karibu saa 4 usiku, kulikuwa na magari kadhaa yaliyokuwa yameegeshwa nje ya hoteli hiyo ispokuwa lile la lakini Toyota Mark X ambalo wanne hao wlaionekana wakitumia mara ya miwsho.

Wapelelezi walisema gari hilo lilipatikana likiwa limefunguliwa na kuongeza kuwa simu za wanaume hao zilikuwa zimezimwa mahali pengine karibu na Everest Park, Barabara ya Mombasa.

Habari Nyingine: Magazeti Jumatano, Aprili 28: Ruto Kutumia Wandani wa Mzee Moi Kumnyorosha Gideon

Kama ilivyoripotiwa hapo awali, wanne hao waliishi maisha ya kifahari na walipenda wanawake na pia walifanya biashara ya kuuza dawa za kulevya.

Kwa upande wake, Elija pia alikuwa akiishi maisha ya kifahari ambayo yaliripotiwa kufadhiliwa na jamaa zake ambao wanaishi ng’ambo. Wanaume hao aidha wanasemakana walikuwa na mazoea ya kukwepa mkono wa sheria.

Maafisa wa polisi sasa wanaendeleza uchunguzi hususan na kampuni ya kuuza magari ambayo wanne hao wanasemekana walikuwa wakijihusiha nayo.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Source: Tuko.co.ke

[ad_2]

Source link