Home » Mauaji Kitengela: Familia ya Jacob Otieno yasema mwili walionyeshwa sio wa jamaa wao ▷ Kenya News
News

Mauaji Kitengela: Familia ya Jacob Otieno yasema mwili walionyeshwa sio wa jamaa wao ▷ Kenya News

Mauaji Kitengela: Familia ya Jacob Otieno yasema mwili walionyeshwa sio wa jamaa wao ▷ Kenya News

[ad_1]

Imebainika kwamba mwili wa mwanaume mmoja uliopatikana katika mto wa Mathioya sio wa yule aliyedhaniwa kuuawa pamoja na marafiki wenzake mtaani Kitengela.

Mauaji Kitengela: Familia ya Jacob Otieno yasema mwili walionyeshwa sio wa jamaa wao
Familia imethibitisha kwamba mwili ambao ulikuwa uliripotiwa kuwa wa Jack Ochieng’ sio wa mpendwa wao.
Source: Facebook

Familia imethibitisha kwamba mwili ambao ulikuwa uliripotiwa kuwa wa Jack Ochieng’ sio wa mpendwa wao.

Kama ilivyoripotiwa awali na TUKO.co.ke, mwili huo ulipatikana na uvunaji mchanga Alhamisi, Aprili 29 na ulichukuliwa na maafisa wa polisi walioupeleka katika hifadhi ya wafu ya hospitali ya Murang’a Level 5.

Familia ya Ochieng’ wakiongozwa na dadake Ndona ambao walifika katika mochuari ya hospitali hiyo kuutambua mwili wake, walisema kwamba mwili huo haukuwa wa Ochieng’.

Kulingana na familia hiyo, Ochieng alikuwa na alama ya kuzaliwa kwenye kifua chake na alikuwa mrefu kwa kimo kuliko mwili walioonyeshwa hospitalini humo.

” Tuliambiwa kwamba mwili ulikuwa umepatikana na kama familia tuliweza kufika kwenye mochuari kuutambua mwili wake, hata hivyo, tumegundua baadaye kwamba sio mwili wa jamaa wetu, Ningependa kujua kakangu yuko wapi, namfahamu vema hakuwa mhalifu,” Alisema Ndona.

Ochieng’, Elijah Obuong, Brian Oduor, na Benjamin Imbai walionekana mara ya mwisho Aprili 19 wakila nyama choma katika klabu ya Enkare mtaani Kitengela.

Taarifa za kuaminika ziliarifu kwamba simu za wanne hao zilizima kuanzia mwendo wa saa nane mchana siku hiyo bila wao kujulikana walipo.

Mwili wa Imbai ulipatika baadaye katika mochuari moja mjini Thika Alhamisi, Aprili 29 ilhali ya Obuong ilipatikana katika mto wa Mukungai ulioko katika barabara ya Murang’a.

Source: Tuko Breaking News Latest

[ad_2]

Source link

About the author

Kenyan Bulletin

I am a young Kenyan interested in new media and dissemination of news and information as it unfolds.