Home » Nyong’o aondoa hofu kuhusu corona inayoshuhudiwa India – Taifa Leo
News

Nyong’o aondoa hofu kuhusu corona inayoshuhudiwa India – Taifa Leo

[ad_1]

Na KNA

GAVANA wa Kisumu Prof Anyang’ Nyong’o, amehimiza wakazi kuondoa hofu kuhusu kuzuka kwa aina ya virusi vya corona – vilivyoathiri watu wengi India – katika kaunti hiyo.

Akihutubia wanahabari Ijumaa, Gavana Nyong’o alisema kuwa Kaunti ya Kisumu haijarekodi kisa chochote kipya cha virusi hivyo tangu raia watano wa India walipopatikana na virusi vya corona mwezi mmoja uliopita.

“Tumeamua kuweka mambo wazi na kutangaza kwamba Kisumu haielekei mkondo wa India. Ni muhimu kuthibitisha kwamba aina ya Covid-19 kutoka India imedhibitiwa na kuangamizwa,” alifichua gavana huyo, ambaye vile vile ni mwenyekiti wa Kamati ya Baraza la Magavana kuhusu Afya.

Katika muda wa siku chache zilizopita, mji huo ulio karibu na Ziwa Victoria, umeripotiwa kuelekea katika hali hatari zaidi baada ya raia watano wa kigeni waliokuwa wakifanya kazi katika kiwanda kimoja kupatikana na aina ya virusi hivyo kutoka India.

Serikali ya Kaunti ilihusisha ufanisi wa kukomesha kusambaa kwa aina hiyo ya virusi kutoka nje ya nchi na juhudi za Idara yake ya Afya iliyochukua hatua haraka kuwaweka waathiriwa karantini iliyolindwa vikali.

[ad_2]
Source link