[ad_1]
– Spika Justin Muturi alifahamisha bunge kuwa Rais amewasilisha jina la Koome kupigwa msasa kuchukua wadhifa wa Jaji Mkuu
– Uhuru alifanya hivyo siku moja tu baada ya JSC kutangaza Koome kuwa mshindi wa mahojiano waliyofanya
– Katiba inahitaji bunge kuidhinisha anayeteuliwa kuchukua wadhifa wa Jaji Mkuu
Rais Uhuru Kenyatta amelitaka bunge kuidhinisha Jaji Martha Koome kama Jaji Mkuu kuchukua viatu vya David Maraga.

Source: Facebook
Rais alikabidhi bunge wasifu na vyeti vya Koome baada ya kuibuka mshindi kwenye uteuzi wa jaji mkuu uliofanywa na Tume ya Huduma za Mahakama (JSC) nchini.
“Rais kwa hivyo anauliza bunge kuidhinisha aliyeteuliwa (kuwa jaji mkuu),” Spika Justin Muturi aliambia bunge Jumatano Aprili 28.
Kulingana na katiba, uteuzi wa Jaji Mkuu unafaa kufanywa na JSC na kisha kupitia kwa rais na bunge ili kuidhinishwa.
Habari Nyingine: Huenda Sisi Ndio Tutaongea na Ruto, Ngunjiri Awaambia Tangatanga
Kaimu mwenyekiti wa JSC Prof Olive Mugenda Jumanne, Aprili 27 alitangaza kuwa tume hiyo ilikubaliana kwa kauli moja kumteua Koome kuwa Jaji Mkuu.
JSC imependekeza kwa kauli moja kumteua Jaji Koome Martha Karabu, jaji wa Mahakama ya Rufani kama Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Kenya,” mwenyekiti wa JSC Olive Mugenda alisema.
Ikiwa ataapishwa, Koome atakuwa Jaji Mkuu wa kwanza wa kike nchini. Hii ni mara ya pili kwa Koome kutafuta wadhifa wa Jaji Mkuu.
Habari Nyingine: Kimeibiwo! Wakili Ngatia Ateta Uteuzi wa Martha Koome kuwa Jaji Mkuu

Source: Facebook
Uteuzi wa Koome hata hivyo umezua hisia mseto huku wakili Fred Ngatia akisema ulikumbwa na udanganyifu.
Ng’atia, ambaye alikuwa anapigiwa upatu na wengi kushinda wadhifa huo, alisema watu fulani wenye ushawishi waliwashinikiza baadhi ya makamishna wa JSC kupunguza alama zake.
Makamishna wanne kutoka eneo la Mlima Kenya walipunguza alama zangu jana mchana baada ya kupigiwa simu na watu wenye nguvu.Bila ya hiyo, nilikuwa nimewashinda waaniaji wengine wote,” alisema.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Source: Tuko
[ad_2]
Source link