[ad_1]
Rais wa Jamhuri ya Burundi Evariste Ndayishimiye na mkewe Angeline Ndayubaha wamewasili mjini Kisumu kwa ajili ya sherehe za Madaraka.

Source: Twitter
Kwa siku mbili ambazo atakuwa humu nchini, Rais Ndayishimiye anatarajiwa kujadili masuala kadhaa ya kibiashara na Rais Uhuru Kenyatta.
Tayari Uhuru amekagua miradi mbalimbali ya maendeleo kwa siku hizi mbili ambazo amekuwa mjini humo.
Kinara wa chama cha ODM Raila Odinga na Waziri wa Mambo ya Nje Raychelle Omamo walimkaribisha Rais Ndayashiye katika uwanja wa kimataifa wa Ndege wa Kisumu.
Baadaye, Rais Uhuru Kenyatta na Mama wa taifa Margaret Kenyatta watawakaribisha viongozi hao katika ikulu ndogo ya Kisumu.
Siku ya Jumanne Juni Mosi, Rais ataongoza hafla hiyo ya Kitaifa itakayofanyika katika Uwanja wa Mamboleo Kisumu, huku mwenzake wa Burundi akiwa mgeni wa heshima.
Source: Tuko
[ad_2]
Source link