Home » COVID -19: Asilimia Mpya ya Maambukizi ni 8.3 Baada ya Visa Vipya 349 Kurekodiwa ▷ Kenya News
News

COVID -19: Asilimia Mpya ya Maambukizi ni 8.3 Baada ya Visa Vipya 349 Kurekodiwa ▷ Kenya News

[ad_1]

– Takwimu mpya za Wizara ya Afya zinaonesha kuwa jumla ya wagonjwa Kenya ni 171,084

– Kati ya visa vipya vilivyorekodiwa watu 327 ni Wakenya nao 22 ni raia wa nchi za kigeni

– Wakati uo huo, wagonjwa 176 wameripotiwa kupata nafuu

Mnamo Jumanne, Juni 1 Kenya ilirekodi visa vipya 349 vya Covid-19, na kufikisha jumla ya wagonjwa nchini hadi 171,084 Waziri wa Afya Mutahi Kagwe amesema.

Habari Nyingine: DP Ruto Apokelewa Kondele kwa Shangwe Kubwa Baada ya Sherehe za Madaraka

COVID -19: Asilimia Mpya ya Maambukizi ni 8.3 Baada ya Visa Vipya 349 Kurekodiwa
Waziri wa Afya Mutahi Kagwe. Picha; MoH.
Source: UGC

Waziri Kagwe katika taarifa yake alithibitisha kuwa idadi hiyo ya wagonjwa ilitokana na sampuli 4,208 zilizopimwa katika saa 24 ambapo kiwango cha maambukizi ni asilimia 8.3.

Kati ya visa vipya vilivyorekodiwa watu 327 ni Wakenya nao 22 ni raia wa nchi za kigeni. Aidha wagonjwa 196 ni wa kiume nao 153 ni wa kike.

Mgonjwa mwenye umri wa chini ni mtoto wa siku saba naye mkongwe alikuwa na miaka 90.

Habari Nyingine: Raila Hakunidai Chochote Wakati wa Handisheki, Rais Uhuru Asema

Jumla ya vipimo tangu kisa cha kwanza kutua Kenya mwezi Machi 2020 imefika 1,815,766.

Idadi ya waliofariki dunia kufikia sasa kutokana na maradhi hayo hatari imefika 3,188 baada ya wagonjwa wengine 16 kupoteza maisha yao kati ya mwezi wa Mei na mwanzoni wa Juni.

Kagwe alisema wagonjwa 1,257 wamelazwa katika vituo mbali mbali vya afya kote nchini na wengine 4,704 wanahudumiwa wakiwa makwao.

Jumla ya wagonjwa 92 nao wamelazwa katika hali mahututi.

Habari Nyingine; Rais Uhuru Kenyatta Aahidi Kuondoa Vikwazo vya Kiuchumi Vilivyowekewa Burundi

Wakati uo huo, wagonjwa 176 wameripotiwa kupata nafuu, 144 kati yao walikuwa wakipokea matibabu manyumbani mwao nao 32 walikuwa wakiunguzwa katika hospitali tofauti tofauti nchini.

Jumla ya waliopata nafuu sasa imefika 117,023, ambapo 85,040 kati yao walihudumiwa manyumbani nao 31,983 walikuwa katika hospitali mbali mbali nchini.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Source: Tuko

[ad_2]
Source link