Home » Kocha Guardiola Avunja Kimya Baada ya Chelsea Kucharaza Man City ▷ Kenya News
News

Kocha Guardiola Avunja Kimya Baada ya Chelsea Kucharaza Man City ▷ Kenya News

[ad_1]

– Guardiola alisisitiza kuwa alichagua kikosi bora kwa fainali ya Ligi ya Mabingwa

– Raia huyo wa Uhispania alishtumiwa vikali kwa kutowahusisha wachezaji wazoefu kwenye safu ya ulinzi wakati wa mechi dhidi ya Chelsea Jumamosi, Mei 29

– Chelsea walichuma nafuu kutokana na kulegea kwa City kwenye safu ya kati kupitia nguli wao N’golo Kante

– Kocha huyo wa Man City alitetea uteuzi wake wa wachezaji akisema anaamini katika ubora wa wachezaji

Habari Nyingine: Europa League: Villarreal Wapiga Man United Kupitia Matuta ya Penalti na Kushinda Taji

Pep Guardiola anasisitiza kuwa alichagua kikosi bora kwa fainali ya Ligi ya Mabingwa licha ya kichapo cha Chelsea siku ya Jumamosi, Mei 29.

Kocha Guardiola Avunja Kimya Baada ya Chelsea Kucharaza Man City
Pep Guardiola alisisitiza kuwa alichagua kikosi bora kwa fainali ya Ligi ya Mabingwa.Picha:Jose Coelho.
Source: Getty Images

City walipigwa 1-0 na miamba hao wa London huku Kai Havertz akifunga bao la kipekee kwenye mchezo huo ambapo kikosi cha Guardiola kilishindwa maarifa.

N’Golo Kante aliibuka shujaa wa mechi hiyo kutokana na kudhibiti safu ya ulinzi kuzuia kikosi cha Manchester City ambacho hakikuwa na uzoefu katika eneo hilo.

Habari Nyingine: Kioja Chazuka Baada ya Mke wa Pasta na Muumini Kuswagana Kanisani

Jambo ambalo lilishtua wengi ni kukosekana kwa nahodha Fernandinho na kiungo wa kati Rodri wakati orodha ya wachezaji ilitangazwa.

Badala yake Guardiola alipendelea huduma za Ilkay Gundogan, Kevin de Bruyne na Bernardo Silva kwenye safu ya mashumbulizi.

Habari Nyingine: Kafyu Yaongezwa Kwa Siku 60, Marufuku ya Kukutana Yawekwa

Kocha Guardiola Avunja Kimya Baada ya Chelsea Kucharaza Man City
Kocha Guardiola hajawahi kushinda tena UEFA tangu 2011 akiwa na Barcelona.Picha:Marc Atkins.
Source: Getty Images

Akizungumza baada ya mechi huyo, raia huyo wa Uhispania alikuwa na ugumu wa kuelezea namna alichagua timu yake.

“Nilijitahidi katika uteuzi. Dhidi ya Lyon [2020] kama ilivyokuwa dhidi ya PSG, Dortmund, nilijaribu kuchagua timu bora kushinda mechi.Wachezaji wanafahamu kama vile Ilkay Gundogan alicheza vizuri,” alisema

Chelsea walichuma nafuu kutokana na kulegea kwa City kwenye safu ya kati huku Mason-Mount akimumegea Kai Havertz pasi ambaye alifunga bao.

Wakati aliulizwa endapo anajutia kuchagua timu hiyo iliyosakata dimba uwanjani Estádio do Dragão, Guardiola badala yake alisifu Chelsea.

“Sijui uamuzi ambao nilifanya lakini wachezaji walifanya kila jitihada kushinda mchezo huo,” alisema.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Subscribe to watch new videos

Source: Tuko

[ad_2]
Source link